Ratiba ya Michuano ya mabingwa wa afrika imetoka ambato tumeshuhudia timu ya Simba sc ikikutana na miamba wa soka kutoka Afrika ya kusini Kaizer Chiefs.
Mechi ya kwanza itapigwa Nchini afrika ya kusini May 14 -15 Katika dimba la johanesburg stadium ambapo Timu ya kaizer chiefs itakua nyumbani ikiwakalibisha wekundu wa mzimbazi kutoka tanzania.
Na mechi ya pili inatarajiwa kupigwa mnamo May 21-22 ,kwenye dimba la Benjamini Mkapa stadium ambapo Simba sc watakuwa wenyeji watakapo wakaribisha Kaizer chiefs katika mechi ya mwisho itakayo amua nani mbabe atakae ingia nusu fainali ,kutokana na agrigate ya mechi ya kwanza.
Simba sc kwasasa wanajiandaa na mechi kubwa ya ligi kuu tanzania bara ambapo itazikutanisha timu mbili mahasimu kutoka tanzania simba sc vs young africans sc itakayopigwa katika dimba la mkapa siku ya tarehe 8 May 2021 ,mchezo unaovuta hisia za mashabiki wengi sana nchini tanzania na afrika kwa ujumla.